Jinsi ya Kuwekeza Soko la Hisa Dar Es Salaam

Tafsiri:

Tangu ilipoanzishwa mwaka 1998, Soko la Hisa la Dar Es Salaam (DSE) ni moja ya chaguzi za uwekezaji zinazopatikana kwa raia na wageni nchini Tanzania. Kulingana na Investment Safety Rankings, Tanzania iko katika nchi 127 kati ya 192 kwa ubora wa kuwekeza, na kuifanya iwe ni ya wastani ukilinganisha na nchi nyingine Afrika. Makala hii kuhusu uwekezaji wa hisa itakuonyesha jinsi ya kuwekeza kwenye Soko la Hisa la Dar Es Salaam.

Nani Anaweza Kuwekeza kwa DSE?

Wote Watanzania na wageni wanaruhusiwa kuwekeza katika soko la hisa Tanzania. Walakini, wageni wanaruhusiwa kuwekeza hadi asilimia 60 katika jumla ya hisa katika kampuni ili kuruhusiwa kujihusisha na biashara ya soko la hisa.

Je Ni Vyombo Vipi Vya Fedha Ambavyo Wafanyabiashara Wanaweza Kununua na Kuuza?

Wafanyabiashara kwenye soko la hisa wanaweza kununua na kuuza hisa, hundi za kampuni na za serikali, n.k.

Hisa Kiganjani: Mwishoni mwa 2020, Sola la Hisa la Dar Es Salaam likishirikiana na Airtel lilizindua mfumo wa kununua hisa mtandaoni kupitia simu janja uitwao ‘simu kiganjani’.

 

Jinsi ya Kununua Hisa

Kwanza, watu wenye nia ya kufanya biashara kwenye soko hili wanatakiwa kufungua akaunti na mmoja wa mawakala 14 wenye leseni.

1. Jaza Fomu ya Ufunguzi wa Akaunti ya CDS

Dalali wako atakupa fomu ya maombi. Mara tu itakapojazwa, utapata nambari ya akaunti ya kwenye mfumo wa elektroniki uitwao Central Depository System (CDS). Biashara zako zote zitarekodiwa kwa DSE kwa kutumia nambari hii.

2. Jaza Fomu ya Ufunguzi wa Akaunti Kwa Dalali

Utahitaji kujaza fomu ambayo inahitaji maelezo ya kibinafsi kama nambari ya kitambulisho, anwani, upendeleo kwa ukusanyaji wa gawio na malipo ya ada. Utahitaji pia kupeleka nakala ya pasipoti yako au leseni ya udereva.

Kwa usajili wa kampuni kwenye soko utahitaji vifuatavyo:

  • Nakala ya cheti cha kusajiliwa kwa kampuni
  • Nakala za vitambulisho vya wakurugenzi wa kampuni
  • Nakala ya katiba ya kampuni
  • Fomu ya maombi ya Akaunti ya amana kwa mwili wa shirika

3. Tuma Fedha Kwa Akaunti ya Dalali Wako

Unahitaji kutuma fedha za kufanyia biashara kwenye soko kwenye akaunti ya dalali. Unaweza kufanya hivyo kupitia benki au njia nyingine yoyote rahisi ya kuhamisha pesa.

4. Peana Agizo la Biashara

Basi unahitaji kuwasiliana na dalali wako kubainisha hisa unayotaka kununua.

Kampuni Kubwa Zilizoorodheshwa

  • Tanzania Breweries (TBL): hisa za TBL ni moja ya hisa kubwa kwenye la soko la hisa DSE na ni mtengenezaji na msambazaji mkuu wa vinywaji nchini Tanzania.
  • East African Breweries (EABL): kampuni ni ya pili kubwa kwenye soko la DSE
  • Acacia (ACA): moja ya wachimbaji wakubwa wa dhahabu nchini Tanzania
  • Tanzania Cigarette Company (TCC): kampuni kubwa kabisa ya tumbaku nchini Tanzania
  • Vodacom (VODA): kampuni kubwa zaidi ya simu nchini Tanzania

Jinsi ya Kununua Hisa za Vodacom

 

Makampuni Yanayouza Hisa Tanzania

Na. Msimbo wa Kampuni Kwenye Soko Kiungo
1 ACA Tazama Wasifu
2 CRDB Tazama Wasifu
3 DCB Tazama Wasifu
4 DSE Tazama Wasifu
5 EABL Tazama Wasifu
6 JHL Tazama Wasifu
7 KA Tazama Wasifu
8 KCB Tazama Wasifu
9 MBP Tazama Wasifu
10 MCB Tazama Wasifu
11 MKCB Tazama Wasifu
12 MUCOB Tazama Wasifu
13 NICO Tazama Wasifu
14 NMB Tazama Wasifu
15 NMG Tazama Wasifu
16 PAL Tazama Wasifu
17 SWALA Tazama Wasifu
18 SWIS Tazama Wasifu
19 TBL Tazama Wasifu
20 TCC Tazama Wasifu
21 TCCL Tazama Wasifu
22 TICL Tazama Wasifu
23 TOL Tazama Wasifu
24 TPCC Tazama Wasifu
25 TTP Tazama Wasifu
26 USL Tazama Wasifu
27 VODA Tazama Wasifu
28 YETU Tazama Wasifu

Hitimisho la Jinsi ya Kununua Hisa DSE

Soko la Hisa la Dar Es Salaam ni mwanachama wa Chama cha Soko la Hisa la Afrika na Shirikisho la Masoko ya Hisa Duniani (WFE). Kwakuwa Tanzania ni sehemu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, DSE, Soko la Hisa la Nairobi na Soko la Hisa la Uganda hatimaye yatakuwa soko moja la hisa la Afrika Mashariki.

Ili kuwekeza katika soko hili, unashauriwa kufanya utafiti wa kina, uwe mwangalifu na uweke malengo ya muda mrefu na usambaze uwekezaji wako ili kupunguza hatari inayotokana na kuwekeza kwenye kampuni moja.

This post is also available in en_US.