Jinsi ya Kuwekeza Katika Soko la Hisa la Nairobi (NSE)

Tafsiri:
en_US

Kenya ni mojawapo ya nchi yenye uchumi wa hali ya juu zaidi barani Afrika. Kenya ina Pato la Taifa la zaidi ya dola bilioni 74. Hii inafanya kuwa nchi ya 9 bora kiuchumi barani Afrika baada ya Afrika Kusini, Nigeria, Misri, Algeria, Moroko, Ethiopia, Ghana, na Angola.

Kenya pia inajulikana kwa sekta yake imara ya kifedha. M-Pesa, bidhaa ya kutuma pesa kwa simu ya mkono inayotolewa na Safaricom, imebadilisha jinsi watu wanavyohifadhi na kutuma pesa. Mtindo wake umekuwa ukiigwa katika masoko mengine mengi yanayoibuka. Kenya pia inajulikana kwa soko la hisa. Katika nakala hii, tutaangalia jinsi ya kuwekeza katika Soko la Hisa la Nairobi (NSE).

Makampuni Katika NSE

  • Jumla ya kampuni 73 zimeorodheshwa katika Soko la Hisa la Nairobi.
  • Kampuni hizi zina thamani ya soko pamoja iliyo zaidi ya dola bilioni 22.
  • Kampuni kubwa iliyoorodheshwa katika Soko la Hisa la Nairobi ni Safaricom ambayo ina dhamana zaidi ya dola bilioni 10.

Soko la Hisa la Nairobi ni Nini?

Ilibadilisha jina lake wakati ilipoanza kuanzisha bidhaa zingine za kuwekeza kam hati ya dhamana au mali isiyoondosheka. Soko la Hisa la Nairobi ni kampuni ambayo huorodhesha hisa zao. Soko la NSE linafanana na masoko kama vile Nasdaq na Soko la Hisa la New York (NYSE).

Makampuni Zilizoorodheshwa Katika Soko la Hisa la Nairobi

  • Kampuni za kilimo kama Sasini na Williamson Teas.
  • Kampuni za magari na vifaa kama Car and General.
  • Benki kama Barclays, Benki ya Equity, na Standard Chartered.
  • Biashara na huduma kama Scan Group na kampuni ya uchapishaji wa Longhorn.
  • Ujenzi na Ushirika kama Bamburi Cement na East Africa Portland.
  • Nishati na Petroli kama Total na Kengen.
  • Kampuni za bima kama Bima ya Jubilee na CIC.
  • Kampuni za uwekezaji kama Centum na Trans Century.
  • Viwanda kama Unga Group na Carbacid.
  • Kampuni za mawasiliano kama Safaricom.
  • Biashara zinazohusisha ardhi na vyumba kama Fahari.
  • Utendaji wa Hisa zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa la Nairobi.

Utendaji wa Soko la Hisa la Nairobi

Hisa iliyoorodheshwa katika Soko la Hisa la Nairobi imekuwa na kipindi kigumu miaka michache iliyopita. Hii ni kwa sababu wawekezaji wengine wa kimataifa wameondoka kwa sababu ya changamoto kubwa za uchumi ambao nchi inakabiliwa nazo.

Gharama ya kufanya biashara inakuwa ghali na kampuni zimekabiliwa na viwango vya juu ya ushuru. Zaidi ya hayo, malipo kwa uelekezi wa viwango vya riba kwa benki vimeathiri utendaji wa Soko la Hisa la Nairobi.

Kama inavyoonyeshwa hapa chini, Nairobi All Share Index (NASI) imepata asilimia 83 tu katika muongo mmoja uliopita. Hii ni asilimia ndogo ukilinganisha na masoko mengine kama vile Dow Jones (DJIA) na S&P.

Nairobi Securities Exchange..
Utendaji wa kampuni zilizoorodheshwa kwenye soko la hisa.

Jinsi ya Kuwekeza Katika Soko la Hisa la Nairobi

Ni jambo gumu kwa wageni wengi kuwekeza katika Soko la Hisa la Nairobi. Hii ni kwa sababu wanahitaji hati kuonyesha kuwa wao ni wawekezaji wa halisi. Lakini, wawekezaji wakubwa wa nje wameona ni rahisi kuwekeza katika soko la hisa nchini Kenya.

Hatua ya kwanza ya kuwekeza katika Soko la Hisa nchini Kenya ni kupata mdalali. Kwa bahati nzuri, kuna wafanyabiashara wengi wa hisa nchini. Benki nyingi huweza kuwa madalali. Madalali wanaoongoza ambao mtu anaweza kutumia ni pamoja na:

  • Madalali wa hisia wa Benki ya Equity
  • Dyer & Blair
  • Suntra Investments
  • NIC Securities
  • Kestrel Capital

Unaweza kupata orodha ya madalali wote nchini Kenya hapa.

Baada ya kupata dalali wako, unapaswa kujiandikisha kwa akaunti ya Kampuni ya Amana ya Kati (CDC). Hii ni akaunti ambayo inaunganishwa na akaunti yako ya uwekezaji. Ni sawa na akaunti ya benki. Lazima ujiandikishe kwa akaunti ya CDC. Ili kufungua akaunti unahitaji kitambulisho chako au nambari ya pasipoti na akaunti yako ya benki.

Mwishowe, baada ya kupata akaunti yako ya CDC, unaweza kumuelekeza mdalali wako anunue hisa unazotaka. Hisa hizi lazima zitanunuliwa kwa kutumia shilingi za Kenya. Unaweza kumuelekeza mdalali kununua hisa hizo kwa kuwaita, kuwatembelea, au mtandaoni. Madalali wengi wa hisa wanatumia mtandao ambapo unaweza kununua na kuuza hisa moja kwa moja.

A chart showing a dashboard of the Nairobi Securities Exchange.

Tamati

Swali kubwa ni kama unapaswa kuwekeza katika Soko la Hisa la Nairobi (NSE) au la. Hili ni swali gumu kujibu kwa sababu ya mwelekeo ambao Kenya inachukua. Nchi imeendelea kuongeza upungufu wake wa deni na bajeti. Wakati huo huo, fedha hizi zimeibiwa na wayahuni. Wakati huo huo, kiwango cha ukosefu wa ajira kinaendelea kuongezeka na serikali imeendelea kupambana – badala ya kusaidia biashara za humu nchini. Bado, unapofanya utafiti wa kutosha, unaweza kupata kampuni zingine nzuri za kuwekeza nchini.