Mambo ya Msingi Unayopaswa Kujua Kuhusu Bima Nchini Kenya

Tafsiri:
en_US

Inasemekana wauzaji wa bima ni wenye hima na wakati mwingine wanaweza kuwa kero wakijaribu kukushawishi uchukue sera ya bima. Wakati wanajaribu kukuuzia sera za bima, inaweza kuonekana kama jambo la kushangaza lakini kuna sababu nyingi kwa nini unahitaji kupata sera ya bima. Hizi ni kati ya sera za bima ambazo zinafaa kuchukua.

1. Bima ya Afya

Bima ya afya inashughulikia gharama za matibabu kwa magonjwa fulani. Unapojeruhiwa au kuugua, kinga ya bima hugharamia matibabu yako. Bima ya afya inashughulikia mambo anuwai. Miongoni mwao ni pamoja na kinga ya kulazwa hospitalini, kinga ya matibabu nje, kinga ya uzazi, kinga ya wenye kipato cha chini, kinga ya wenye kipato cha juu na ya kati.

Kinga ya Matibabu ya Ndani

Kinga ya matibabu ya ndani inashughulikia gharama zote za matibabu unapolazwa hospitalini. Hii itajumuisha dhima inayohusiana na kulazwa hospitalini kama vile malazi na gharama za matibabu ya moja kwa moja. Ili kutoa madai, bima itakuhitaji kupata kibali kutoka hospitalini kwamba ugonjwa wako unahitaji ulazwe hospitalini.

Kinga ya Matibabu ya Nje

Kinga hii inagharamia matibabu ya nje. Mwenye wa sera hutafuta huduma kutoka kwa hospitali au kliniki ambayo imethibitishwa na bima. Hivyo kinga hii inamsaidia mtu ambaye anaumwa ila anatibiwa na kurudi nyumbani. Kinga hii ni bei rahisi ukilinganisha na kinga ya matibabu ya ndani.

Kinga ya Uzazi

Kinga hii inabeba gharama za kulazwa hospitalini na kujifungua. Pia inashughulikia matukio mengine ambayo yanaweza kuja kutokana na ujauzito.

Kinga ya Wenye Kipato Cha Chini

Kinga hii imeanza kutolewa hivi karibuni na kampuni za bima. Sera hiyo inalenga watu katika maeneo yenye kipato kidogo. Kinga hii ina malipo ya chini, na inakusudia kusaidia wamiliki wa sera kupata huduma za matibabu za ndani na nje. Kati ya sera za bima kwa wenye kipato cha chini nchini Kenya ni Bima ya Jamii.

Kinga ya Wenye Kipato Cha Kati na Juu

Kinga hii hulipwa na waajiri kwa wafanyakazi wao. Inafanya kazi kwa njia ambayo ikiwa mfanyakazi akiumia wakati anafanya kazi anapata fidia. Sera hii ni sehemu ya malipo ya wafanyakazi. Wafanyakazi walio na vyeo vya juu hupata kinga ya gharama kubwa, wakati wafanyakazi wa vyeo vya kati wanapata kinga ya gharama ya kati.

The Insurance Regulatory Authority is a statutory government agency established under the Insurance Act.

2. Bima ya maisha

Sera ya bima ya maisha hutoa usalama wa kifedha kwa mtu ambaye umemtaja kama mnufaishwa pale utakapofariki. Sera ya bima ya maisha haitoi tu kinga ya maisha yako, lakini inajumuisha pia athari za kifedha zinazotokana na kifo chako. Pia inashughulikia gharama za mazishi, gharama za masomo zilizopangwa, mapato yaliyopotea na pia madeni. Unaweza kuchukua bima ya maisha hadi umri fulani au bima ya maisha ya muda fulani.

Bima ya Maisha Hadi Umri Fulani

Bima hii ni hadi umri fulani ambapo mwenye bima hulipa malipo kwa miaka kadhaa na kisha kupata kinga maisha yake yote . Ikiwa kifo cha mmiliki inakuja kwanza kabla ya kufiia umri uliotajwa na kinga, fedha zake na bonasi yake hulipwa kwa mnufaika. Aina hii ya bima ina thamani ya kusalimisha fedha, ambayo ni baada ya miaka mitatu wakati unalipa malipo.

Bima Maisha ya Muda Fulani

Sera hii ndio mashuhuri sana nchini Kenya. Malipo ya kulipwa kwa kipindi maalum. Bima nyingi hulipa mtu kwa vipindi na malipo ya mwisho hulipwa muda wa mwisho wa sera. Sera ya hii ina jumla ya malipo yaliyothibibitishwa na thamani ya kusalimisha fedha baada ya miaka mitatu ya malipo. Jumla ya malipo yaliyothibitishwa hulipwa kwa mnufaika baada ya muda wa sera.

3. Bima ya Gari

Ni lazima kwa watu binafsi kuhakikisha magari yao nchini Kenya yana bima. Sera za bima ya gari nchini Kenya ni za aina tatu. Aina hizi ni pamoja na kinga ya mhusika wa tatu, wizi wa mhusika wa tatu na moto na kinga kamili.

Bima ya Mhusika wa Tatu

Hii ni bima ya msingi ya magari nchini Kenya. Ni lazima kwa kila dereva kuwa na bima hii. Bima hii inashughulikia mhusika wa tatu katika masuala ya dhima kutokana na ajali. Inalinda mhusika wa wa tatu kutokana na majeraha ya mwili na uharibifu wa mwili wa gari. Kinga hii hailindi mmiliki kutokana na upotezaji wa fedha au kuumia kwa mwili.

Bima ya Wizi wa Mhusika wa Tatu na Moto

Hii ni aina nyingine ya sera ya bima inayotolewa nchini Kenya. Sera inatoa kinga dhidi ya wizi na moto. Bima pia inakulipia ikiwa gari lako litaharibiwa kwa sababu ya jaribio la wizi. Kwa mfano, ikiwa kioo cha gari kitavunjika wakati wa jaribio la kuiba, bima itafidia gharama za ukarabati. Sera itakununulia gari jingine ktokana na uharibifu wa moto au wizi.

Sera Yakinifu ya Bima

Bima hii ndio bima pana zaidi nchini Kenya. Sera inashughulikia hatari anuwai za kifedha ambazo dereva anaweza kukutana nazo. Faida ya kinga hii ni kwamba inamlida dereva, dhima ya mhusika wa tatu, wizi wa mhusika wa tatu na wizi. Pia inajumuisha kinga kutoka na ajali nyingine kama kugongwa, majanga ya asili kama vile maporomoko ya ardhi.

Hitimisho

Kuchukua sera ya bima ni muhimu kukulinda kutokana na upotezaji wowote wa kifedha. Pia itahakikisha wanufaia wako watafaidika ikiwa utafa. Kampuni nyingi za bima nchini Kenya zinatoa huduma tofauti za bima. Tafuta bima ambayo itafikia mahitaji yako ya bima kabla ya kuchukua sera.