Jinsi ya Kupata Mkopo Kenya [Mkopo wa Simu]

Kuna wakati unahitaji fedha kwa haraka ili kutatua jambo fulani. Unaweza kuomba msaada toka kwa marafiki au ndugu. Hata hivyo wanaweza wasiwe na uwezo wa kukusaidia. Kwa bahati nzuri, unaweza kuomba mikopo binafsi au mikopo ya biashara toka benki au kampuni ya mikopo mtandaoni. Ukiacha benki, hizi ni huduma nyingine unazoweza kutumia kwa mikopo kwa njia ya simu nchini Kenya. Hii ni mikopo ya haraka bila dhamana.

M-Shwari

M-Shwari ni huduma ya mikopo ya haraka kupitia simu inayotolewa kupitia M-Pesa. Huduma hii ni ushirikiano kati ya Safaricom and Benki ya CBA iliyoanzishwa mwaka 2012. Kupata mkopo unatakiwa uwe na umri wa miaka 18, uwe tayari na akaunti ya M-Pesa kwa kipindi cha miezi 6.

Kiwango cha chini cha mkopo ni Ksh 100 na kiwango cha juu ni Ksh 20,000. Mkopo una kipindi cha siku 30 cha kulipa kwa riba ya 7.5%. Unaweza kulipa mkopo kupitia akaunti yako ya M-Pesa. Ikiwa siku 30 zimepita, malipo yatatolewa kwenye akaunti yako ya M-Shwari. Ukichelewa kulipa utatakiwa kulipa 7.5% ya kiwango kilichobaki kumaliza malipo.

KCB M-Pesa

Huduma hii ni ya ushirikiano kati ya Safaricom na Benki ya Kenya Commercial (KCB). Kiwango cha chini cha mikopo ya pesa ni Ksh 50 na kiwango cha juu ni Ksh 1,000,000. Itakubidi uwe na KCB M-Pesa menu kwenye simu yako.

Kupata mkopo inakubidi uwe na miaka 18 au zaidi, uwe na akaunti ya M-Pesa kwa kipindi cha miezi 6, Historia yako ya akaunti ya M-Pesa ndio itakadiria kiwango cha mkopo utakachopewa.

mikopo binafsi

MCo-op Cash

MCoop cash ni huduma ya mkopo inayotolewa na Co-operative Bank of Kenya kwa kutumia "app". Kiwango cha chini cha mkopo ni Ksh 3,000 na kiwango cha juu ni Ksh 100,000.

Ili uweze pata mkopo kwa simu toka MCo-op cash unahitajiwa kuwa mteja wa Cooperative Bank. Unahitaji pia kupata "app" toka the Google Play Store au the iOS Store. Mkopo wa binafsi mwezi mmoja una riba ya 1.166% wakati mkopo wa binafsi wa miezi mitatu una riba ya 3.498%. Mkopo wa biashara una riba ya 1.166% na mkopo wa bima wa miezi mitatu una riba ya 0.102%.

Eazzy Loan

Eazzy loan ni huduma ya mkopo wa pesa ya Equity Bank. Unahitaji kuwa mteja wa Equity Bank. Unahitaji pia kuwa na kadi ya simu ya Equitel. Kuna aina mbili za mikopo toka Eazzy Loan: Mkopo wa Benki ya Equity na mkopo wa Eazzy plus. Toka Eazzy Plus unaweza kukopa hadi Ksh 3,000,000. Kiwango cha chini cha Mkopo wa Benki ya Equity ni Ksh 100 na kiwango cha juu ni Ksh 200,000.

Mkopo wa Benki ya Equity una kipindi cha miezi 12 cha kulipa wakati Eazzy Plus ni siku 30. Riba ya mikopo hii ni kati ya 2% na 10% ikijumisha malipo mengine ya benki, kodi, n.k.

Mikopo ya Branch (Branch Loan)

Branch, ilianzishwa mwaka 2015 huko San Francisco ikiwa na ofisi Nairobi. Wakenya wengi wamekuwa wakitumia huduma hii kupata mikopo. Kupata mkopo toka Branch unahitaji kuwa mteja wa M-Pesa na uwe na akaunti ya Facebook yenye jina linalofanana na jina kwenye kitambulisho chako cha serikali. Kampuni hii pia ni moja ya app za mikopo Tanzania.

Hivi ndivyo jinsi ya kupata mkopo Branch. Unatakiwa upate app ya Branch toka Google Play Store kisha uiunge na akaunti yako ya Facebook. Kisha weka maelezo yanayotakiwa kama vile namba ya simu. Kiwango cha chini cha mkopo ni Ksh 1000 na kiwango cha juu ni Ksh 50,000. Mkopo hutolewa kupitia M-Pesa na riba inategemea na kipindi cha kulipa mkopo wako. Fuata kiungo hiki ujue jinsi ya kulipa mkopo Branch.

Tala Loan

Tala, iliyoanzishwa mwaka 2014, ilikuwa ikiitwa Mkopo Rahisi. Kupata mkopo toka Tala, unahitaji kuwa rekodi nzuri ya M-Pesa na pia uwe na simujanja. Kiwango cha mkopo kinategemea historia ya matumizi yako ya M-Pesa. Unaweza pia kukopa Airtel Money kupitia Tala.

Unachotakiwa kufanya ni kupata ""app"" ya Tala toka Google Play Store kisha uiunge na akaunti yako ya Facebook kisha uweke maelezo yanayohitajika. Kiwango cha chini cha mkopo ni Ksh 500 na kiwango cha juu ni Ksh 50,000 ambapo riba ni 15%. Utalipa mkopo wako kwa muda wa wiki tatu kupitia M-Pesa.

Timiza Loan (Jinsi ya Kupata Mkopo wa Timiza)

Timiza ni "app" ya Benki ya Absa. Huduma hii inapatikana kwa yeyote mwenye simu. Sio lazima uwe mteja wa benki hii. Unaweza kutumia hii ""app"" kutunza fedha zako ili kuweza kupata kiwango cha juu cha mkopo hapo baadaye. Jinsi ya kupata mkopo wa Timiza hata kama huna simujanja ni kwa kupiga namba hii *848#.

mKey

Finserve Africa ilianzisha huduma ya mKey Kenya kama mapinduzi ya huduma za fedha zinazomjali mteja. Kwa kutumia "app" hii unaweza pia kutuma fedha kwenye huduma ya M-Pesa, Equitel Money na Airtel money. Unaweza pia kununua muda wa kuongoea toka kampuni za simu za Safaricom, Equitel, Airtel, Telkom na Faiba. Licha ya kupata mikopo ya haraka kwenye simu, unaweza kutumia huduma hii kulipa na kununua bidhaa na huduma.

Hitimisho Mkopo wa Pesa Kenya

Kabla ya kuamua kutumia huduma zilizotajwa hapo juu kupata mkopo wa haraka kwa njia ya simu, hakikisha kuwa unajua kiwango cha riba, muda wa kulipa na mashari ya kupata mkopo wa binafsi au wa biashara. Hii itakusaidia kupata mikopo kwa njia ya simu bila kuwa na matatizo mbeleni wakati wa kulipa.

Habari za Nyongeza Kama Unataka Mkopo

  • Jinsi ya kukopa Airtel Money na mkopo Mpesa kupitia M-Fanisi
  • Jinsi ya kukopa Airtel kupitia Kopa Chapaa