Mikopo ya Haraka Kwenye Simu na Mtandao Afrika Mashariki

Kutokana na mapinduzi ya teknolojia za pesa kupitia simu za mkononi kama vile Mpesa, siku hizi ni rahisi kupata mikopo ya haraka bila dhamana Tanzania, Kenya, Rwanda, Uganda na kwingineko. Hivyo unaweza kupata mikopo kwa njia ya simu, mikopo mtandaoni au mkopo kwa njia ya SMS. Wenyeji bila dhamana au kuhitaji kujaza fomu. Baadhi ya mifano katika makala hii ni miongoni mwa taasisi ambazo unaweza kupata mikopo ya haraka bila dhamana 2022.

Ingawa ni rahisi kukopa kwa njia ya simu, lazima uwe mwangalifu kwani baadhi ya kampuni za mikopo hutumia mbinu za unyanyasaji na vitisho wakati wanafuatilia malipo ya mkopo. Moja ya mbinu wanazotumia ni kuwasiliana na watu unaofahamiana nao kuwaambia kuwa hutaki kulipa mkopo wako ili kukuabisha. Kabla ya kuomba mkopo, tafuta watu wengine ambao wameitumia kampuni ya mikopo unayotaka kuitumia ili ufahamu uhusiano wao na wateja wao.

 

Kampuni Zinazoto Mikopo ya Papo Hapo

Kuna kampuni mbalimbali ambao zinatoa mikopo ya haraka kupitia simu. Kampuni hizo ni pamoja na hizi:

Tunakushauri kuchukua mkopo baada ya kujaribu vyanzo vingine vya kupata pesa kama vile ndugu na marafiki au kutunza fedha kila mwezi ili kufikia kiwango cha pesa unachohitaji. Ni bora uchukua mkopo kwa ajili ya kuimarisha biashara yako. Kamwe, usichukue mikopo kwa ajili ya starehe. Usijaribu hata kidogo.

HaloYako (Tanzania)

Halo Loan ni mkopo wa muda mfupi kupitia simu ya mkononi uliobuniwa na Benki ya FINCA Microfinance kwa kushirikiana na Halotel kwa ajili ya wateja wa HaloYako. Zaidi ya mikopo, HaloYako inawawezesha watumiaji kuhifadhi fedha zao (Halo Savings). Ada ya mikopo ya HaloYako ni asilimia 10 kwa mkopo wa mwezi mmoja. Ukiwa na sifa zinazotosha, ukiomba mkopo utaupata bada ya dakika chache tu. Kwa mkopo wako wa kwanza, utaweza kupata kiwango cha chini cha shilingi 2,000 wakati kiwango cha juu ni 15,000.

Ili kupata mikopo ya haraka bila dhmana Tanzania, lazima uwe mteja wa Halotel uliyesajiliwa katika huduma za HaloPesa. Ombi la mkopo binafsi bila dhamana likiidhinishwa, kiwango kilichotolewa kitatumwa moja kwa moja kwenye mkoba wako wa HaloPesa. Ili mteja wa HaloYako aweze kuipata lazima atumie huduma za HaloPesa. Ukiwa ni mteja wa HaloPesa jisajili na HaloYako kwa kupiga kwenye simu ya HaloPesa *150*88# na kuchagua 7. Kumbuka kuwa ili kuhitimu Mkopo wa Halo, unahitaji kuwa mtumiaji aliyesajiliwa wa huduma za HaloYako na kuwa mtumiaji wa huduma za HaloPesa.

Kukopa Halotel: Watu wengine hutaka kujua jinsi ya kukopa Halotel. Kwa bahati mbaya, hivi sasa hakuna mikopo ya Halotel. Kampuni hii haijaanza kutoa mikopo moja kwa moja zaidi ya mikopo ya HaloYako ambayo hutumwa kwenye mikoba ya HaloPesa.

Tigo Pesa Nivushe (Tanzania)

Utaweza kupata huduma ya Tigo ivushe ukikidhi vigezo. Wateja waliosajiliwa wa Tigo Pesa wanaotumia Tigo Pesa kwa miamala mbalimbali na matumizi ya simu za mkononi wanaweza kukopa kiasi cha kuanzia TZS 1,000 hadi TZS 2,000,000 kulingana na mahitaji na ustahiki wao.

Jinsi ya Kukopa Tigo Nivushe

Tigo inatoa mikopo kwa wateja ambao hutumia huduma za muda wa maongezi, intaneti, meseji, malipo ya bili na huduma mbalimbali za Tigo Pesa. Utapokea meseji pindi utakapokidhi vigezo vya kupata mkopo. Ili kukidhi vigezo vya mkopo, endelea kutumia huduma za Tigo na Tigo Pesa mara kwa mara.

Kujiunga na Tigo Pesa, piga *150*01#, chagua 7 huduma za kifedha kisha chagua 4 Mikopo na kisha Tigo Nivushe kwenye laini yako ya Tigo kisha chagua 1. Itakupasa ukubali marejesho ya ndani ya siku 30 na kisha kuchagua kiwango cha mkopo unachohitaji bila kuzidisha kiwango ulichopewa na Nivushe. Kisha utaingiza namba ya siri. Kama utapata meseji kuwa haujakidhi vigezo, basi utakuwa hauwezi kupata mkopo bado. Ili kukidhi vigezo vya mkopo, endelea kutumia huduma za Tigo na Tigo Pesa mara kwa mara.

Tigo Bustisha (Tanzania)

Bustisha ni huduma ya mkopo inayokuwezesha kukamilisha miamala (transactions) yako ya Tigo Pesa ikiwa hauna pesa za kutosha kwenye akaunti yako ya Tigo Pesa. Wateja wote wa Tigo Pesa wanastahili kupata huduma hii baada ya kujisajili.

Baada ya muamala kushindikana kutokana na kutokuwa na pesa za kutosha kwenye akaunti yako, kama umejiunga na Tigo Bustisha, utapokea taarifa ya kikomo cha Bustisha unachotakiwa kuongezewa ili kukamilisha muamala huo, na ombi la idhini yake ya kutumia huduma hii. Baada ya kukubali, muamala utakamilika na fedha zitatumwa moja kwa moja kwa mlengwa. Mteja akikataa, muamala utakataliwa na mteja atapewa taarifa ya kutokuwa na salio la kutosha. Unatarajiwa kurejesha pesa uliyoongezewa baada ya kuweka au kupokea pesa kwenye akaunti yako ya Tigo Pesa.

Jinsi ya Kukopa Tigo Bustisha

Kukopa Tigo Bustisha, unalazimika kwanza kujisajili na kukubali kutumia huduma ya Bustisha kupitia menyu ya Tigo Pesa au kwenye App ya Tigo Pesa. Hivyo kujiunga na Bustisha, piga *150*01#, chagua 7 Huduma za Kifedha, chagua 4 Mikopo, chagua 2 Bustisha, kubali Vigezo na Masharti, ingiza namba ya siri kuthibitisha

M-Pawa (Tanzania)

M-Pawa ni huduma ya kibenki ya Vodacom na CBA ambayo inakuwezesha kuhifadhi pesa kwenye simu, kupata riba kutokana na akiba na kupata mikopo ya haraka kwa M-Pesa Tanzania. Kiasi cha chini cha mkopo ni shilingi 1000.

Jinsi ya Kujiunga na M-Pawa

Sifa zinazohitajila ili kupata mkopo wa M-Pawa ni kuwa lazima uwe mteja wa Vodacom na umekamilisha usajili na pia uwe na akaunti ya M-Pesa inayofanya kazi. Unatakiwa uwe na moja ya vitambulisho vifuatavyo: pasi ya kusafiria ya Tanzania, kitambulisho cha taifa, kitambulisho cha kupiga kura, leseni ya udereva, kitambulisho cha kazi au barua kutoka serikali za mitaa.

Timiza (Tanzania)

Timiza Mkopo ni huduma ya mkopo bila dhamana au akiba Tanzania toka kwa kampuni ya Airtel. Hii ni moja ya mikopo ya papo kwa hapo Tanzania yenye kiwango cha riba nafuu. Kiasi cha mkopo kinategemea matumizi yako ya pesa ya Airtel. Unaweza kukopa kiasi kikubwa kila wakati unapolipa mikopo yako kwa wakati.

Jinsi ya Kupata Mkopo wa Timiza

Ili kuhitimu mkopo wa Timiza unahitaji kuwa mteja wa Airtel Money na uwe na vigezo vifuatavyo:

  • Uwe zaidi ya umri wa miaka 18
  • Umejisajili kama mteja wa Airtel kwa siku 90+
  • Uwe na akaunti hai ya Airtel Money
  • Usiwe na mkopo wa JUMO wakati wa maombi
  • Usiwe na tabia mbaya ya malipo na JUMO

Ukiwa na sifa hizo, kupata mkopo wa Timiza piga *150*60# na uchague chaguo 4 kwenye menyu kuu ya Airtel Money. Utahitaji kuingiza PIN yako ya Airtel Money ili kukubali Sheria na Masharti ya Timiza. Baada ya hapo, nenda tu kwa chaguo 1 kwenye menyu kuu ya Huduma ya Mkopo wa Timiza na uchague Omba Mkopo.

Mikopo ya Tala Tanzania: Hakuna tena mkopo wa Tala Tanzania hivi sasa. Wateja ambao bado wanadaiwa wanaweza kulipa mikopo yao kwa kutumia Tigo-Pesa namba 888000 and nambari ya simu uliojisajilia na Tala kama akaunti yako. Hata hivyo, mikopo ya Tala Kenya bado inapatikana. Soma makala yetu hii kuhusu jinsi ya kupata mkopo wa Tala Kenya.

M-Koba (Tanzania)

M-Koba ni huduma ya Vodacom kwa kushirikiana na TPB Bank ya kutunza fedha, kupeana mikopo na kugawana faida kwa vikundi kama familia na marafiki, VICOBA, VSLA, SACCOS, Upatu na vikundi mbalimbali vyenye Utamaduni wa kuchanga kwa lengo la kuweka akiba na kukopeshana pesa.

Hakuna ada inayopatikana na mteja wakati wa kutuma pesa kutoka kwa mkoba wao wa M-Pesa kwa akaunti ya akiba ya kikundi cha M-Koba. Kwa kutumia simu ya mkono, kila mshiriki anaweza kuomba kutazama fedha za akiba ya kikundi au maafisa wa kikundi, ambao ni mwenyekiti, katibu na mweka hazina. Kila mshiriki anaweza kuomba mikopo moja kwa moja kwa kutumia USSD. Washiriki watatu wa kikundi watateuliwa na teknolojia ya M-Koba bila mpangilio maalum ili kuidhinisha mikopo kabla ya kutolewa.

Jinsi ya Kujiunga na MKoba Vodacom

Kujiungana M Koba kunafanya kupitia USSD na kiongozi wa kikundi. Akaunti ya M-Koba inamruhusu kiongozi huyo kuongeza washiriki kwenye kikundi kwa kutumia nambari zao za rununu. Kwa taarifa zaidi kuhusu jinsi ya kujiunga na kunufaika, soma hapa.

Saida Mkopo ni moja ya kampuni zilizokuwa zikitoa mikopo kwa njia ya simu Tanzania. App ya Saida mkopo haipatikani tena.

Branch Mkopo (Tanzania/Kenya)

Branch ni moja ya app za mikopo Tanzania inayotoa mikopo ya haraka kwenye simu nchini Tanzania na pia Kenya. Programu ya Branch ya Android inapatikana kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza. Kutumia Branch kwa lugha ya Kiswahili, hakikisha kuwa una toleo la mwisho la programu yake kisha nenda kwenye “My Account”, halafu bonyeza “App Settings”, kisha nenda kwenye “Language”, na uchague “Kiswahili” na mwishowe bonyeza “Submit”.

Jinsi ya Kuomba Mkopo Branch

Unaweza kupata mkopo hadi shilingi 700,000. Kupata mkopo wa haraka kwa njia ya simu toka Branch ni rahisi. Hivyo, kama unataka mkopo online, hivi ndio jinsi ya kupata mkopo Branch:

  • Pata programu ya Branch ya Android
  • Akaunti ya Facebook
  • Kitambulisho cha taifa, kadi ya mpiga kura au leseni ya udereva
  • Namba ya mkoba wa fedha wa simu (mobile money wallet)
  • Ruhusa kwa Branch ili waweze kuingia ndani ya simu yako ili kujua aina ya simu unayotumia, data na pia kusoma SMS zako. Hii inasaidia kampuni kujua kiasi cha mkopo unachoweza kupewa

Ukifuata hatua hizo basi utaweza pata mkopo kwa simu Tanzania. Branch ni kati ya kampuni zinazotoa mikopo ya haraka Tanzania kwani maombi yako yakifanikiwa, utapata mkopo kati ya masaa 3 hadi masaa 24. Hivyo ukitaka mikopo ya papo kwa papo, tunakushauri ujaribu kampuni ya Branch.

Tunakushauri kuchukua mkopo baada ya kujaribu vyanzo vingine vya kupata pesa kama vile ndugu na marafiki au kutunza fedha kila mwezi ili kufikia kiwango cha pesa unachohitaji. Ni bora uchukua mkopo kwa ajili ya kuimarisha biashara yako. Kamwe, usichukue mikopo kwa ajili ya starehe. Usijaribu hata kidogo.

M-Shwari (Kenya)

Huu ni mkopo kwa simu ambao unatokana na ushirikiano kati ya Safaricom na Commercial Bank of Africa (CBA). Mbali na muundo wake wa amana, M-Shwari inatoa mikopo ya kati ya shilingi 1000 na milioni moja. kwa watumiaji wa M-Pesa. Kiwango cha juu cha mikopo kinategemea kiwango cha udeni wa mtu binafsi, na hutozwa riba ya asilimia 7.5. Ni moja ya mfumo maarufu wa mikopo ya mitandaoni nchini. Takriban asilimia 30 ya Wakenya ambao wanamiliki simu za mkononi wamewahi kukopa fedha kutoka mfumo huu na CBA imeidhinisha zaidi ya mikopo 50,000 kila siku.

Jinsi ya Kuomba Mkopo wa M-Shwari

  • Nenda kwenye menyu ya M-Pesa kwenye simu yako na uchague Mikopo na Akiba
  • Chagua M-Shwari na kisha Mikopo
  • Omba mkopo kwa kuingiza kiasi unachotaka kabla ya kuweka PIN yako ya M-Pesa
  • Fedha hizo zitatumwa moja kwa moja kwenye akaunti yako ya M-Pesa

Fuliza na M-Pesa: Fuliza ni mpango wa “overdraft” wa kampuni ya Safaricom. Ikiwa unafanya shughuli na M-Pesa lakini fedha kwa mkoba wako wa M-Pesa hazitoshi, unaweza kupata fedha kupitia Fuliza ili ukamilishe shughuli yako. Fedha utakazopata zitategmea kiwango unachostahili kutokana na matumizi yako ya M-Pesa. Kujiandikisha, piga simu *234# na uchague Fuliza. Unahitajiwa kuwa tayari ni mteja wa M-Pesa.

Tala (Kenya)

Mikopo ya mkononi ya Tala, ambayo awali ilikuwa inajulikana kama Mkopo Rahisi. Hutoa mkopo wa haraka kwenye simu hadi shilingi 50,000.

mikopo ya haraka online
Programu ya mkopo ya Tala.

Jinsi ya Kupata Mkopo Tala

Hatua zifuatazo ndio jinsi ya kupata Tala mkopo online:

  • Pakua programu ya Tala kutoka Google Play Store
  • Sajili akaunti. Kwa kufanya hivyo, utahitaji akaunti ya M-Pesa na pia nambari ya pasipoti au kitambulisho cha kitaifa.
  • Nenda kwenye “Apply Now” na ujibu maswali yaliyowasilishwa
  • Chagua kipindi cha malipo ambayo yanakufaa
  • Bonyeza “Send My Loan”. Fedha zitatumwa kwa akaunti yako ya M-Pesa papo hapo.

MoKash Loan Uganda

MoKash ni huduma ambayo inawaruhusu wanachama wake kuhifadhi na kupata mkopo wa haraka bila dhamana. Tangu kuanzishwa kwa mpango huu mwaka wa 2016, wateja wake wamekuwa wakiongezeka kwa kasi. Kila mkopo unaoidhinishwa hutozwa ada ya mara moja tu ya asilimia 9. Ili uweze kufuzu kwa ajili ya mkopo kwenye mfumo huu, akaunti yako ya pesa ya MTN ya inastahili kuwa hai kwa angalau miezi 6 iliyopita. Zaidi ya hayo, unapaswa kuwa mtumiaji wa MoKash ikiwa ni pamoja na kuhifadhi kiasi kikubwa katika akaunti yako.

 

Jinsi ya Kuomba Mkopo Kwa Njia ya Simu ya Mkononi toka MoKash

  • Bonyeza `*165*5#Y` kuanzisha MoKash
  • Nenda kwa ‘Savings and Loans’ na kisha uchague ‘Loans’
  • Nenda kwa ‘Request a Loan’
  • Weka kiasi cha fedha unachotaka kukopa
  • Weka nambari yao ya siri
  • Utapata ujumbe wa kuthibitisha kuwa maombi yako ya mikopo ya papo hapo yamefanikiwa na fedha zimetumwa kwa akaunti yako

BK Quick Loan Rwanda

Huu ni mkopo wa haraka wa kwenye simu ulioanzishwa na Benki ya Kigali. Mkopo wa BK Quick Rwanda ulianzishwa kwa nia ya kutoa jukwaa rahisi kwa wateja wake kufikia baadhi ya huduma za benki hiyo. Mtu anaweza kupata mikopo ya pesa hadi RWF milioni 1 na kurejesha kwa muda wa miezi 1 hadi 12. Kila mkopo wa mkononi hutozwa riba ya asilimia 4. Mkopo uliotolewa hutumwa kwa akaunti ya BK ya mteja. Hakuna ada zinazotozwa kwa ajili ya uhamisho wa fedha kati ya BK Quick na akaunti za BK.

online mobile loans east africa
Mikop ya BK Quick nchini Rwanda.

Jinsi ya Kutuma Maombi ya Mkopo wa BK Quick

  • Sajili namba yako ya simu kwa huduma ya BK MobiServe
  • Piga *334*
  • Nenda kwa ’10 -BK Quick ‘
  • Fuata maagizo na ukubali sheria na masharti yaliyotolewa
  • Fedha zitatumwa mara moja kwenye akaunti yako ya BK

Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Kuomba Mkopo Bila Dhamana

Kuomba mkopo kwa njia ya simu ni rahisi sana. Huhitaji kondoka nyumbani kwako au sehemu yako ya biashara ili kwenda kuomba mkopo. Unachohitaji ni simu ya mkono. Pia, hakuna haja ya kujaza fomu. Hata hivyo, urahisi huu unaweza kukuletea matatizo baadaye kama hutatazama mambo makuu ya kuzingatia. Mambo hayo ni pamoja na haya:

  • Kufikia data (access to data). Kampuni hizi huhitaji ruhusa ili kuingia ndani ya simu yako na kupata data mbalimbali. Data hizi huwasaidia kuweza kufikia uamuzi wa kuwa utaweza kukipa mkopo au la. Data wanazochukua toka kwenye simu yako ni pamoja na GPS (ili kujua unatembelea sehemu gani, maduka gani na hoteli unazotembelea, n.k. na kuweza kujua wewe ni mtu wa daraja gani katika jamii). Kampuni hizi pia zitachukua rekodi ya watu ambao umekuwa mkipigiana simu au kutumiana ujumbe wa maandishi, kitabu cha orodha ya namba za simu, historia yako na kampuni za pesa za simu za mkono kama vile Mpesa na Airtel Money ili kujua kiwango cha shughuli zako za pesa na kampuni hizi, n.k.
  • Kiwango cha riba (interest). Tazama kiwango cha riba ambacho kampuni itakuhitaji kulipa wakati unalipa mkopo wako. Kampuni nyingi hutoa mikopo yenye riba kati 7% hadi 15% kwa kila mwezi. Hii inamaanisha kuwa ukijumlisha riba ya mkopo kwa mwaka mzima utakuwa umelipa riba kubwa sana kuliko aliyepata mkopo kutoka benki.
  • Ada ya huduma (service fee). Baadhi ya kampuni huwa na ada ya kukuhudumia. Ada hii huweza kujumuishwa kwenye kiwango cha mwisho unachohitajiwa kulipa. Hivyo, unaweza kudhani kuwa utalipa mkopo na riba kumbe kuna pia ada ya huduma! Kampuni nyingi hutoza ada ya 10% hivi kwa ajili ya huduma zao.
  • Malipo ya adhabu ya kuchelewa kulipa deni (late payment penatly). Mara nyingi, kampuni za mikopo hukutoza ada ambayo ni adhabu kwa kuchelewa kulipa mkopo wako.
  • Soma Kanuni na Masharti ya mkopo (Terms and Conditions). Watu wengi hukubali masharti ya kubonyeza “ndio” bila kuyasoma. Ni muhimu sana usome Kanuni na Masharti ya mkopo la sivyo utajilaumu bure baadaye.
  • Ofisi za mikopo (credit bureau). Moja ya masharti ya kampuni hizi ni kuwa zina haki ya kukuripoti kwenye ofisi za mikopo jambo ambalo litakuharibia rekodi yako ya mikopo na kufanya iwe vigumu kwako kupata mikopo kwa urahisi baadaye.

Hitimisho Kuhusu Mikopo ya Haraka Bila Dhamana Kwa Simu na Mtandaoni

Mkopo wa haraka bila dhamana kwa simu na mkopo mtandaoni ni huduma ya kifedha ambayo unaweza kupata kupitia kampuni tulizoorodhesha hapa. Kampuni hizi zinazotoa fedha kwa wateja papo hapo kwa kiwango cha chini cha riba. Kumbuka kuwa ingawa ni rahisi kukopa kwa njia ya simu, lazima uwe mwangalifu kwani baadhi ya kampuni za mikopo hutumia mbinu za unyanyasaji na vitisho wakati wanafuatilia malipo ya mkopo.

Tunakushauri pia ni bora uchukua mkopo kwa ajili ya kuimarisha biashara yako au shughuli nyingine muhimu sana. Kamwe, usichukue mikopo kwa ajili ya starehe.

Habari Zaidi