Jinsi ya Kununua na Kuuza Bitcoin Kwa M-Pesa

Tafsiri:
en_US

Kununua Bitcoin, hakuhitaji mtu kuwa na fedha nyingi. Kwa bahati nzuri, hata kwa dola moja, bado waweza kununua sarafu za kidijitali. Sarafu za kidijitali ni fedha zenye thamani sawa na fedha za kawaida. Lakini ni kwa vipi waweza kuuza na kununua bitcoin kwa M-Pesa?

Soma makala hii kwa Kiingereza: How to Buy Bitcoin with Mpesa

Kununua Bitcoin kwa M-Pesa

Yakubidi ufuate hatua zifuatazo ili kununua sarafu mtandao kwa M-Pesa:

  • Tembelea duka la kubadilisha fedha za kidijitali kama vile Yellow Card, jisajili bure na unda akaunti.
  • Baada ya kujiunga, chagua mfanyabiashara anayekidhi matakwa yako, kwa mfano baadhi ya wauzaji wana wastani wa chini wa shilingi 1,000 za Kenya, wakati wengine wana wastani wa chini wa shilingi 10,000 za Kenya. Kisha angalia sifa za muuzaji huyo kabla hujanunua. Hakikisha unafanya biashara na wafanyabiashara wenye asilimia alama mia moja ya mrejesho.
  • Pindi umuaminipo muuzaji, bonyeza ‘buy Bitcoin’ mbele ya jina lake ili kununua. Tovuti itakuelekeza kwenye ukurasa wenye vigezo na masharti. Soma vigezo na masharti ya mfanyabiashara huyo.
  • Baada ya kukubaliana na vigezo na masharti ya mfanyabiashara, ingiza kiasi unachotaka kubadili kuwa Bitcoin kwa shilingi ya Kenya. Utaziona kiasi cha Bitcoin utakazopokea.
  • Kisha fanya malipo kwa kutumia M-Pesa na kisha thibitisha kiasi. Mara utapokea Bitcoin.

Hakikisha unafanya biashara na wafanyabiashara wenye asilimia alama mia moja ya mrejesho (feedback).

Jinsi ya Kutoa (Withdraw) Bitcoin kwa M-Pesa

Inawezekana kutoa Bitcoin kwa kutumia M-Pesa. Yaani una Bitcoin kisha unazibadili ili ziwe shilingi. Hii ndiyo njia rahisi ya kufanya. Mtambue muuzaji wa Bitcoin anayeaminika na anayejishughulisha na utoaji wa Bitcoin kwa M-Pesa. Mtumie Bitcoin unayotaka kuitoa. Wao watakutumia pesa taslimu kwenye M-Pesa inayowiana na Bitcoin uliyotuma. Hapo waweza kutoa pesa hiyo kwa M-Pesa.

Ni lazima ujifunze mambo muhimu ya sarafu mtandao ambayo mara kwa mara utakuwa unayatumia.

  • Mkoba wa bitcoin: Mboba wa bitcoin au wallet ya bitcoin ni mfuko wa kidijitali kwa utunzaji wa sarafu mtandao. Mfuko huo una chaguo la kutuma, kupokea na kuhuisha (backup) sarafu zako. Ili kupokea fedha kwenye mfuko wako, unahitaji kumpa mtumaji anuani ya mfuko wako. Anuani ya mfuko wako ni kama namba ya akaunti ya benki au namba ya M-Pesa. Chukua tahadhari kuhuisha usiri wa mfuko wako pamoja na vibonye umma nje ya mtandao kwa usalama.
  • Soko la bitcoin (Cryptocurrency exchange): Hili ni soko ambapo watu huuza na kununua bitcoin mtandaoni. Watu hawahitaji kuonana kwa vile wanaweza kubadilishana fedha za kidijitali kwa njia ya mtandao. Nchini Kenya na Tanzania, kuna masoko mengi ya kuuza na kununua fedha ambayo mtu aweza kuyatumia.

Maduka ya Kuuza na Kununua Fedha za Kidijitali (Wakala wa Bitcoin

Kuna masoko maarufu ambayo mtu aweza kununua na kuuza sarafu za kidijitali kwa kutumia M-Pesa. Hayo ni pamoja na:

Bitnob ni kampuni ya Bitcoin iliyoanzisha huduma zinazowawezesha watumiaji wake nchini Kenya kutuma na kupokea Bitcoin kwenye akaunti zao za Mpesa. Unaweza pia kubadili Bitcoin zako ili upate Shilingi ya Kenya kwenye akaunti ya TKASh na Airtel Money. Unaweza pia kutumia Bitnob kupokea pesa toka kwa ndugu na marafiki wanaoishi Marekani ya nchi kupitia app za Strike na Cash App.

Paxful

 jinsi ya kununua bitcoin tanzania

Paxful ni duka maarufu ambalo mtu aweza moja kwa moja kununua fedha za kidijitali kwa kutumia M-Pesa nchini Kenya. Pindi ujisajilipo, waweza kununua au kubadilisha Bitcoin kwa kutumia M-Pesa. Lina mchakato rahisi na wa haraka wa kujiisajili. Ni sehemu nzuri zaidi ya biashara ya fedha za kidijitali, kwa vile ina sehemu ya huduma ya msaada kwa wateja na pia uwepo wa jumuiya ya watumiaji wa Bitcoin barani Afrika.

Yellow Card

Yellow Card ni moja ya masoko bora kwa watu wasio na uzoefu mkubwa wa masuala ya bitcoin na sarafu za dijitali kwa kutumia Mpesa. Ni moja wa wakala wa bitcoin Tanzania na nchi nyingine kama Kenya, Rwanda na Uganda. Matumizi ya soko hili ni mepesi kujifunza ili kununua, kuuza na kuhifadhi bitcoin zako.

Moja ya uzuri wa soko la kununua na kuuza bitcoin la Yellow Card ni kuwa kampuni hii ina ofisi Dar Es Salaam, Tanzania na Nairobi, Kenya. Hii ni tofauti na kampuni nyingine zilizoorodheshwa hapa ambazo zinapatikana mtandaoni lakini ofisi zake ziko nje ya nchi.

Unachotakiwa kufanya kabla ya kununua bitcoin kupitia Yellow Card Tanzania ni kuunda akaunti yako kupitia tovuti yake au app yake ya Android na iOS. Njia za kulipa au kupokea malipo au kubadilisha bitcoin ili upate shilingi ni pamoja na M-Pesa.

LocalBitcoins

LocalBitcoins ni soko linaloshughulika na sarafu za kidijitali aina ya Bitcoin pekee. Unahitajika kujisajili kwanza na kuamilisha akaunti kwa kupitia kiungo kinachotumwa kwenye barua pepe yako ili kuanza. Ukimaliza hayo, waweza kuabiri na kutafuta nyasifu za wafanyabiashara ambao utafanya nao biashara.

Pursa

Pursa ni kati ya wakala wa bitcoin wanaokupa soko la kununua na kuuza bitcoin. Kwenya soko la Pursa, unaweza kununua na kuuza kwa kutumia njia mbalimbali za malipo ikiwemo M-Pesa.

LocalCryptos

LocalCryptos ni duka ambalo hapo nyuma lilikuwa likiitwa Localethereum. Kwenye eneo hili, waweza fanya biashara ya kununua na kuuza bitcoin kwa kutumia M-Pesa. Kwa bahati nzuri, kuna huduma ya utawala wa kifedha wa mtu wa tatu iitwayo escrow ambayo inatumika kuhakikisha fedha muuzaji wa bitcoin hatoweki na fedha zako baada ya kulipa.

Soma makala yetu kuhusu jinsi ya kununua Bitcoin Tanzania. Makala hii itakuonyesha masoko makuu ya kununua bitcoin nchini Tanzania. Pia soma jinsi ya kuwekeza Bitcoin.

Hitimisho Kuhusu Jinsi ya Kununua Bitcoin

Fedha za kidijitali ni tete. Inakubidi uzinunue baada ya utafiti yakinifu na kwa tahadhari. Kumbuka kutowekeza kiasi cha fedha usichopenda kukipoteza. Ukifuate mwongozo huu utajuaa jinsi ya kununua Bitcoin Tanzania na nchi nyingine ambazo zina Mpesa.