Wakati bitcoin inaendelea kupata umaarufu barani duniani, tunapenda kukusaidia kujua wapi unaweza kununua bitcoin Tanzania. Hivyo, mwongozo huu utakusaidia kujua jinsi ya kujiunga na bitcoin Tanzania.
Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan ya jana Juni 13, 2021 kuhusu sarafu za mtandaoni imeipa fursa sarafu ya Bitcoin baada ya kutoa habari njema kwa soko hilo. Hotuba yake huko Mwanza ilifuata baada ya nchi ya El Salvador kutangaza kupitisha Bitcoin kama njia halali ya malipo ya zabuni sambamba na mataifa mengine ya Amerika Kusini na Kati kuonyesha utayari wao wa kutumia sarafu hiyo. — Gazeti la Mwananchi.
Yaliyomo
Bitcoin Ni Nini? Cryptocurrency ni Nini?
- Cryptocurrency ni fedha dijitali. Zipo cryptocurrency nyingi ile bitcoin ndio maarufu zaidi na yenye uhakika na usalama zaidi. Bitcoin ni fedha dijitali isiyosimamiwa na benki kuu au msimamizi mmoja ambayo inaweza kutumwa kutoka kwa mtumiaji mmoja hadi mwingine kwenye mtandao wa bitcoin.
- Bitcoin ilianzishwa mnamo 2008 na mtu asiyejulikana au kikundi cha watu kwa kutumia jina la Satoshi Nakamoto na ilianza mnamo 2009.
- Bitcoin huweza kubadilishwa kwa sarafu zingine, au kununua bidhaa na kulipia huduma kama vile shilingi.
- Bitcoin huhifadhiwa kwenye mkoba wa bitcoin (waleti ya bitcoin) unaotunzwa kwenye kompyuta au simujanja yako.
Unachohitaji Kabla ya Kununua au Kuuza Bitcoin
Watu wengi huenda Google kuuliza eti jinsi ya kujiunga na bitcoin Tanzania. Bitcoin sio chama au kikundi ambacho unaweza kujiunga nacho. Bitcoin ni fedha, hivyo unaweza kuinunua au kuiuza ila sio kujiunga nayo.
Kama ilivyoelezwa hapo juu, shughuli za bitcoin zinahitaji mkoba wa bitcoin (waleti ya bitcoin). Kununua bitcoin Tanzania utahitaji soko (cryptocurrency exchange) la ambalo watu wanaweza kununua na kuuza bitcoin (orodha ya wakala wa bitcoin Tanzania iko hapo chini).
Kisha utahitaji fedha za kawaida kama shilingi (ikiwa unataka kununua) au bitcoin (ikiwa unataka kuuza). Kama shughuli zingine za jadi za kifedha, lazima uchague njia yako ya malipo unayopendelea kama vile M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money, kadi ya benki, uhamishaji fedha kwa kutumia benki, na huduma za kimataifa kama vile Western Union, Moneygram, Transferwise, fedha taslimu, n.k.
Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Kununua au Kuuza Bitcoin Tanzania
Unapotaka kununua au kuuza bitcoin, unahitaji kuzingatia mambo kadhaa muhimu. Wakati wa kuchagua soko la bitcoin, hakikisha unafanya bidii inayofaa ili kujua, kwa mfano, sifa ya soko hilo katika tasnia ya Bitcoin, ni lini ilisajiliwa, ni nani watendaji wake, jiulize kama imekata bima kutunza fedha za wateja wake, nk.
Sehemu nyingine muhimu ya habari unayohitaji kujua ni ada zao. Angalia ada zao za kununua na kuuza, ada ya uondoaji wa bitcoin toka kwenye akaunti, ada ya amana, n.k. Zaidi ya hayo, ni vyema ujue kikomo cha kiwango cha bitcoin unachoweza kununua au kuuza. Kiwango hutofautiana kati ya soko na soko.
Ikiwa unaamua kutumia soko linalowawezesha watu wawili kununua na kuuziana bitcoin moja kwa moja (peer to peer), unahitaji kuwa mwangalifu zaidi kwa sababu kwa chaguo hili utakuwa unafanya biashara yako na mtu usiyemjua. Tafuta ikiwa mtu huyo anayekuuzia bitcoin maelezo yake binafsi katika soko analotumia yamethibitishwa, jinsi gani anaaminika kwenye soko hilo (tazama maoni ya watu wengine walionunua bitoin toka kwake), n.k. Ikiwa lazima ukutane na muuzaji wa bitcoin ana kwa ana, chagua mahali pa umma na uombe rafiki au jamaa aende nawe.
Wakati wa kuchagua mkoba wa kuhifadhi Bitcoin, unahitaji kuzingatia mambo kama usalama wake, matumizi ya neno la siri, uwezo wa mkoba kuficha taarifa zako (ikiwa unataka kufanya biashara ya bitcoin bila kujulikana) na masoko ambapo mkoba huo unaweza kutumika. Soko la kununua au kuuza Bitcoin utakalochagua linaweza pia kupendekeza mkoba wa kutumia. Soma makala hii yenye orodha ya waleti imara za bitcoin.
Bei ya bitcoin inatofautiana ulimwenguni na hubadilika mara kwa mara. Unaweza kutumia CoinDesk kufanya ulinganisho wa bei ili kujua bei nzuri ya kununua bitcoin.
Jinsi ya Kununua Bitcoin Tanzania na Jinsi ya Kuuza Bitcoin Tanzania
Ili kuweza kuuza au kununua bitcoin Tanzania, unatakiwa kuchagua soko (bitcoin exchange) utakalotumia. Yafuatayo ni masoko makuu na yanayoaminika ya kununua bitcoin Tanzania.
Yellow Card Tanzania
Yellow Card ni moja ya masoko bora kwa watu wasio na uzoefu mkubwa wa masuala ya bitcoin na sarafu za dijitali nchini Tanzania. Matumizi ya soko hili ni mepesi kujifunza ili kununua, kuuza na kuhifadhi bitcoin zako.
Moja ya uzuri wa kutumia Yellow Card kama wakala wa bitcoin Tanzania ni kuwa kampuni hii ina ofisi Dar Es Salaam, Tanzania. Hii ni tofauti na kampuni nyingine zilizoorodheshwa hapa ambazo zinapatikana mtandaoni lakini ofisi zake ziko nje ya nchi.
Unachotakiwa kufanya kabla ya kununua bitcoin kupitia Yellow Card Tanzania ni kuunda akaunti yako kupitia tovuti yake au app yake ya Android na iOS. Njia za kulipa au kupokea malipo au kubadilisha bitcoin ili upate shilingi ni pamoja na M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money au benki za KCB, DCB au NCBA.
Remitano Tanzania
Unaweza pia kuchagua kwenda na kampuni ya Shelisheli inayoitwa Remitano. Inatoa soko la kuaminika la bitcoin ambalo watu hununua na kuuza Bitcoin nchini Tanzania.
Pursa Tanzania
Pursa ni kati ya masoko ya kununua na kuuza bitcoin Tanzania bila matatizo. Kwenya soko la Pursa, unaweza kununua na kuuza kwa kutumia njia mbalimbali za maliko zikiwemo Ezy Pesa, Airtel Money, MasterCard, Halotel Money, Tigo Pesa, Visa, au TTCL. Kwenye soko hili, huhitaji kujiandikisha ili ununue au uuze bitcoin.
Paxful ilikuwa ni moja ya kampuni maarufu duaniani kwa kuuza na kununua bitcoin. Mnamo Aprili 4, 2023, kampuni hii ilitangaza kuacha kufanya biashara.
Coinmama Tanzania
Coinmama ilianzishwa mwaka 2013 na hadi sasa imetoa huduma kwa wateja zaidi ya milioni 2 million katika nchi zaidi ya 180 ikiwemo Tanzania. Ukitumia Coimama unaweza kulipa kwa kutumia kadi za benki, benki, n.k.
CEX.io
CEX.IO ni ulingo unaokuwezesha kununua na pia kuuza bitcoin Tanzania. Kununua bitcoin Tanzania kupitia CEX.io unaweza kulipa kwa kutumia benki, kadi ya benki au huduma kama vile Skrill. Ukinunua bitcoin kupitia soko hili unaweza kubadilisha bitcoin zako kwenda kwa shilingi kwa kutumia akaunti yako ya benki.
Soma pia: Jinsi ya Kununua Bitcoin Kwa M-Pesa
Hitimisho Kuhusu Jinsi ya Kununua Bitcoin Tanzania
Bitcoin 1 ililingana na shilingi 79,057,198.50 za kitanzania mnamo Juni 25, 2021. Tanzania haijazuia rasmi Bitcoin. Walakini, benki kuu haidhibiti biashara ya Bitcoin. Ukifuata mwongozo huu utaweza kununua bitcoin Tanzania na kushiriki kwenye biashara ya bitcoin Tanzania kikamilifu. Lakini, unatakiwa kuwa makini maana kuna matapeli wengi wa bitcoin.